Picha: RC TELACK AFUNGUA MKUTANO WA WADAU KUJADILI MAPENDEKEZO YA SHERIA NDOGO KUBORESHA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO

Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack amefungua mkutano wa wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto kwa ajili ya kujadili Mapendekezo ya sheria ndogo za vijiji/halmashauri za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto katika halmashauri za wilaya mkoa wa Shinyanga.

Mkutano huo uliolenga kujadili kwa pamoja mikakati inayolenga kuboresha huduma za afya ya uzazi na mtoto ili kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wachanga,umefanyika leo Jumatatu Juni 3,2019 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga.

Telack alisema ili kuondoa vifo hivyo ni vyema akina mama wajawazito wanahudhuria kliniki akibainisha kuwa pia ni jukumu la baba kumhamasisha mkewe kuhudhuria kliniki na kujifungulia kwenye vituo vya afya.

“Takwimu za mwaka 2018 zinaonesha kuwa vifo vitokanavyo na uzazi mkoani Shinyanga vilipungua hadi 56 kutoka vifo 73 mwaka 2017,vifo vya watoto wachanga vilipungua kutoka 915 mwaka 2017 hadi 913 mwaka 2018”,alieleza.

“Ingawa takwimu za vifo zinaonesha kupungua.Nia ya serikali ni kuhakikisha mama mjamzito anajifungua salama na mtoto wake anakua,Sote tutambue kuwa hakuna mama anayestahili kufa wakati wa uzazi wala mtoto mchanga,hivyo ni lazima wadau wote tusongeze jitihada,mikakati na rasilimali ili kuhakikisha tunakuwa na vifo 0”,aliongeza Telack.

Mkuu huyo wa mkoa alisema,Rasimu ya mapendekezo ya uundwaji wa sheria ndogo za kuboresha afya ya uzazi na mtoto imejumuisha mawazo kutoka kwa watendaji wa sekta ya afya ngazi za halmashauri na kusititiza kuwa sheria ndogo zitakazoundwa zisikinzane na Sheria mama,sera na miongozo katika sekta ya afya.

“Ninafurahi kuona kwamba moja ya mkakati katika makubaliano yetu wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya ‘Jiongeze Tuwavushe Salama’ unatekelezwa.Nawaelekeza wanasheria wa halmashauri na Mwanasheria wa mkoa ambao pia ni washiriki wa mkutano huu kutumia weledi wao kushauri na kuhakikisha kwamba kazi hii inakamilika kwa wakati”,aliongeza.

Akiwasilisha rasimu ya sheria ndogo za vijiji/halmashauri za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto,Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt.Rashid Mfaume alivitaja visababishi vinavyochangia vifo vya mama na mtoto kuwa ni kutokuhuduria kliniki kwa wakati na mfumo dume unaosababisha mwanamke kutokuwa na maamuzi.

Alisema sababu zingine kuwa ni kutokufuata ushauri unaotolewa na wataalamu,mila na desturi potofu pamoja na jamii kukosa elimu ya kutosha kuhusu dalili za hatari za mjamzito,mzazi ana watoto wachanga.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akifungua mkutano wa wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto ili kujadili Mapendekezo ya sheria ndogo za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto katika halmashauri za wilaya mkoa wa Shinyanga. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack akizungumza katika mkutano wa wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto.Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Jasinta Mboneko,kulia ni Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela.
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto ili kujadili Mapendekezo ya sheria ndogo za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto katika halmashauri za wilaya mkoa wa Shinyanga.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt.Rashid Mfaume akiwasilisha Mapendekezo/rasimu ya sheria ndogo za vijiji/halmashauri za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto,Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Jasinta Mboneko akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto ili kujadili Mapendekezo ya sheria ndogo za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto katika halmashauri za wilaya mkoa wa Shinyanga.
Mratibu wa Huduma za afya ya uzazi na mtoto mkoa wa Shinyanga,Joyce Kondoro akitoa taarifa ya huduma za afya ya mama na mtoto mkoa wa Shinyanga.
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela akiongoza majadiliano wakati wa mkutano wa wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto ili kujadili Mapendekezo ya sheria ndogo za uboreshaji wa huduma za afya ya uzazi na mtoto katika halmashauri za wilaya mkoa wa Shinyanga.
Wadau wa huduma za afya ya uzazi na mtoto wakiwa ukumbini.
Wadau wakiwa kwenye mkutano huo.
Wenyeviti wa halmashauri za wilaya wakiwa ukumbini.
Mkutano unaendelea.
Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kishapu,Boniface Butondo akizungumza wakati wa mkutano huo.
Mkuu wa wilaya ya Kahama,Anamringi Macha akichangia hoja wakati wa mkutano huo.
Katibu Tawala Msaidizi Serikali za Mitaa Mkoa wa Shinyanga,Alphonce Kasanyi akitoa ufafanuzi kuhusu masuala ya sheria.

Mwenyekiti wa wanasheria wa serikali mkoa wa Shinyanga, Stephen John Magalla akielezea mchakato wa uundwaji sheria ndogo za vijiji na halmashauri.
Mkurugenzi wa shirika la  DSW, Peter Owaga akichangia hoja kwenye mkutano huo.
Mkurugenzi wa halmashauri ya Msalala Simon Berege akichangia hoja ukumbini.

Wadau wakiwa ukumbini.

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Jasinta Mboneko akiwa ukumbini.
Mkutano unaendelea.
Wadau wakiwa ukumbini.
Mkutano unaendelea.
Wadau wakiwa ukumbini.

Mkuu wa wilaya ya Kahama, Anamringi Macha akiwa ukumbini.
Mkutano unaendelea.
Katibu Tawala mkoa wa Shinyanga,Albert Msovela na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Dkt.Rashid Mfaume wakiteta jambo ukumbini.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post