TRUMP KASEMA KILICHOMFANYA ASIISHAMBULIE KIJESHI IRANI NI KUHOFIA VIFO VYA WATU 150.....JANA IRAN ILIITUNGUA NDEGE MOJA YA MAREKANI


Rais wa Marekani Donald Trump amesema leo kuwa alisitisha shambulizi la kijeshi dhidi ya Iran kwa sababu jibu kama hilo kwa hatua ya Iran kutungua ndege ya Marekani isiyoruka na rubani lingesababisha idadi kubwa kabisa ya vifo. 

Katika mfululizo wa ujumbe aliondika kwenye mtandao wa Twitter, Trump amesema vikwazo vya kiuchumi vya Marekani dhidi ya Iran vinafanya kazi na vingine vimetangazwa jana usiku kufuatia kuharibiwa kwa ndege ya Marekani isiyoruka na rubani iliyotunguliwa na kombora la Iran.

Trump amesema mpango ulikuwa ni kulipua maeneo matatu tofauti ya Iran kama jibu la kitendo cha Iran, na kuwa aliambiwa watu 150 wangeuawa na ndio maana akasitisha shambulzii hilo zikiwa zimesalia dakika 10 tu kwa ndege za Marekani kufyatua makombora.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527