MWANAFUNZI CHUO KIKUU CHA KAMPALA TAWI LA TANZANIA (KIU) AFARIKI DUNIA KWA KUCHOMWA VISU NJE YA GETI LA CHUO

Mwanafunzi wa stashahada ya maabara kutoka Chuo Kikuu cha Kampala tawi la Tanzania (KIU), Anifa Mgaya amefariki dunia  Jumapili usiku baada ya kushambuliwa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali na watu wasiojulikana.




Anifa alikutwa na umauti majira ya saa 2 usiku jirani na geti la kuingia katika chuo hicho kilichopo GongolaMboto jijini Dar es Dar es Salaam alichokuwa akisoma.

Taarifa zinaeleza baada ya kushambuliwa, wanafunzi wenzake walijitokeza ili kumpatia msaada kwa kumkimbiza hospitali lakini hadi wanafika alikuwa tayari umauti umemfika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Zuberi Chembela alithibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akibainisha vijana waliohusika katika tukio hilo wanasemekana kuwa ni vibaka.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527