MBUNGE JAGUAR WA KENYA ALIYETISHIA KUWATIMUA WATANZANIA AKAMATWA

Maafisa wa polisi nchini Kenya wamemkamata mbunge wa jimbo la Starehe anayedaiwa kutoa kauli za chuki dhidi ya wafanyabiashara wa Tanzania na Uganda waliopo jijini Nairobi.


Vyombo vya habari vya nchi hiyo vinaripoti kuwa Charles Kanyi maarufu kama Jaguar amekamatwa mchana huu akiwa anatoka kwenye viwanja vya bunge.


Jana, June 25 Serikali ya Kenya ilitoa taarifa ya kuwahakikishia wafanyabiashara wa kigeni nchini humo usalama wakati wote huku ikisema Serikali haipo upande wa Mbunge wa Starehe, Charles Njagua maarufu Jaguar kuhusu kauli alizozitoa.


Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki kupitia mitandao ya kijamii jana Jumanne ilisambaa video yake akieleza kuwafukuza wafanyabiashara wa kigeni wakiwemo Watanzania ndani ya masaa 24 kurudi kwao la sivyo watawapiga na kuwarudisha nchini mwao..




Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527