AFISA MTENDAJI WA KIJIJI AUAWA KWA KUSHAMBULIWA NA WASIOJULIKANA


Picha haihusiani na habari hapa chini

Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ibambilo Kata ya Bulega Wilayani Bukombe Mkoani Geita,Juma Maziku, amefariki dunia saa chache baada ya kuokotwa akiwa ametupwa kwenye barabara iendayo Mnekesi Wilayani Chato,huku mwili wake ukiwa na majeraha ya kushambuliwa na watu wasiojulikana.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita amesema kitendo hicho hakikubaliki na kuahidi kuwasaka na kuwakamata wale wote waliohusika na tukio hilo.

"Kitu alichofanyiwa mtumishi huyu wa wananchi hakikubaliki kabisa, likemewe na kila mtu na kama kamati ya Ulinzi hatutafurahia inajurudia tena, tutahakikisha tunafanya msako ili watuhumiwa wachukuliwe hatua za kisheria." amesema DC Mkumba

Aidha,Mkuu huyo wa Wilaya amesema matukio kama hayo yanasababishwa na baadhi ya watumishi wa umma kuishi mbali na vituo vyao vya kazi na kuagiza ifikapo tarehe moja mwezi wa saba kila mtumishi awe amehamia na kuishi anakofanyia kazi.
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527