LUGOLA ATANGAZA KIAMA KWA POLISI WASIOTII MAAGIZO YAKE

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amesema kuanzia Juni 15, 2019 ataanza ziara katika vituo mbalimbali vya polisi kukagua utekelezaji wa agizo lake kuhusu jeshi hilo kuzishikilia pikipiki (Bodaboda).

Aametoa kauli hiyo leo ambapo ameeleza kuwa atapita kila kituo kwa nyakati tofauti kuangalia utekelezaji wa agizo hilo, huku akisisitiza kuwa anataka suala hilo liishe ili tuondoe malalamiko ya muda mrefu ya vijana kuhusu bodaboda zao.

“Nawaambia nikikuta kituo chako kuna bodaboda  umezikamata tofauti  na makosa niliyoanisha ile kauli ya niliyoisema Bungeni itatimia siku hiyo,” anasema Lugola.

Utakumbuka May 20, 2019 akiwa Bungeni Lugola alitoa maagizo kwa polisi akitaka pikipiki zinazokamatwa na kuwekwa vituoni ni zile zilizohusika katika uhalifu, zilizoibiwa na zisizo na wenyewe badala ya kuziweka kituoni bodaboba zenye makosa ya kofia ngumu au kupakia abiria zaidi ya watatu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post