URUSI YAIONYA MAREKANI DHIDI YA KUJIINGIZA KIJESHI VENEZUELA

Rais Vladimir Putin wa Urusi ameonya dhidi ya Marekani kuivamia kijeshi Venezuela na kusema hilo litakuwa balaa kubwa. 

Rais Putin amekumbusha washirika wa Marekani hawaungi mkono jambo hilo. 

Akizungumza katika kongamano la kiuchumi la mjini St. Petersburg, Rais Putin amesema pia kwamba wataalam wa kiufundi wa Urusi wanasalia Venezuela ili kushughulikia mitambo ya kijeshi ya Urusi, jambo ambalo anasema wanalazimika kulifanya. 

Hata hivyo, anasema Moscow haifungui kituo chochote cha kijeshi nchini Venezuela.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post