LORI LAGONGA TRENI DODOMA....WATU 29 WAJERUHIWA


Watu 29 wamejeruhiwa baada ya lori kugonga treni jijini Dodoma. Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Protas Katambi amesema leo asubuhi Jumanne Juni 18, 2019 kuwa ajali hiyo imetokea jana saa 5.30 usiku.


Amesema ametoa maagizo kwa vyombo vya usalama kumsaka dereva wa lori ambaye inasemekana aliruka kutoka kwenye lori baada ya ajali hiyo kisha kutokomea kusikojulikana.

Shughuli ya kuondoa mabehewa ya treni inaendelea huku ulinzi ukiwa umeimarishwa katika eneo la tukio huku polisi waliokuwa na silaha wakiwa wameimarisha ulinzi katika tukio.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527