KESI YA UCHOCHEZI INAYOMKABILI TUNDU LISSU YAPIGWA KALENDA


Kesi ya uchochezi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu na wenzake watatu imeahirishwa baada ya mbunge huyo kuendelea na matibabu nje ya nchi.

Mbali na Lissu washtakiwa wengine ni Mhariri wa Gazeti la Mawio Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh wanaokabiliwa na kesi ya uchochezi..

Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde amedai mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Juni 24,2019 kuwa shauri lilikuja kwa ya kutajwa na aliomba ipangwe tarehe nyingine.

Baada ya maelezo hayo Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba amesema washtakiwa wote wataendelea na dhamana yao na  shauri hilo limeahirishwa hadi Julai 24, 2019 kwa ajili ya kutajwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527