BABA ADAIWA KUBAKA NA KULAWITI BINTI YAKE

NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA
JESHI la polisi mkoani Pwani,linamshikilia Suleiman Issa Ngorombwe (43) mfanyabiashara na mkazi wa Mailmoja Tangini ,Kibaha,kwa kudaiwa kumbaka na kumlawiti binti yake wa miaka 11.


Kamanda wa polisi mkoani Pwani,Wankyo Nyigesa alieleza kwamba,tuhuma ziliripotiwa katika kituo cha polisi Kibaha Mjini Juni 20 majira ya asubuhi ambapo walimkamata mtuhumiwa.

"Baada ya upelelezi wa tuhuma hii kukamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani "

Alieleza,jeshi la polisi linaendelea kukemea vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia na vya kinyama vinavyofanywa na baadhi ya watu kwenye jamii.

Wankyo alisema,vitendo vya aina hiyo huanzia ngazi ya familia hivyo alitoa rai kwa wananchi kutoa ushirikiano wa kuripoti taarifa za matukio kama hayo ili wahusika wachukuliwe hatua za kisheria na iwe fundisho kwa wengine.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527