WAZIRI MBARAWA ATEUA WAKURUGENZI WATATU


Waziri wa Maji Prof. Makame Mbarawa,  Mei 16, 2019 amefanya uteuzi wa Wakurugenzi watendaji watatu wa mamlaka za maji safi na usafi wa mazingira.

Taarifa iliyotolewa na katibu mkuu wa Wizara hiyo Prof. Kitila Mkumbo imeeleza kuwa walioteuliwa ni Mhandisi Mbike Jones Lyimo ambaye atakuwa Mkurugenzi wa KUWASA mkoani Kigoma.

Mwingine ni Bi. Flaviana Kifizi, ambaye amekuwa mkurugenzi wa SHUWASA mkoa wa Shinyanga.

Wa tatu katika walioteuliwa ni Mhandisi Robert Lupoja ambaye anakuwa mkurugenzi wa MUWASA huko Musoma mkoani Mara.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527