MADEREVA WA MALORI YA MAFUTA WAPONGEZA WAKALA WA VIPIMO 'WMA" KUWAFUNGULIA KITUO CHA KUPIMA MAFUTA MISUGUSUGU


Na Emmanuel Mbatilo
Madereva wa Malori ya Mafuta (Trucker) wameishukuru taasisi ya Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) kwa kuwafungulia kituo cha kupima mafuta kilichopo Misugusugu mkoani Pwani kwa kuwa kimewasaidia kupunguza kero ya kusubiri kupima kwa muda mrefu.

Wamesema uanzishwaji wa kituo hicho umeleta tija kwa sababu kimepunguza sana msongamano wa maroli wakati wa kupima mafuta

Wamesema awali walikuwa wakipima katika kituo cha Ilala ambacho eneo lake ni finyu sana hivyo ilikuwa vigumu sana kupima kwa haraka jambo ambalo lilikuwa likileta kero kwa wasafirishaji wa mafuta.

Kituo hicho kinapima zaidi ya Magali 60 kwa siku kuliko hapo mwanzo katika kituo kilichopo Ilala.

Wamezungumza hayo wakiwa katika harakati za upimaji wa magari yao Misugusugu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527