TUNDU LISSU KUREJEA NCHINI SEPTEMBA 7


Mbunge Tundu Lissu amesema atarejea nchini Septemba 7, 2019, siku ambayo itatimia miaka miwili tangu aliposhambuliwa kwa risasi jijini Dodoma Septemba 7, 2017, Lissu ambaye yuko nchini Ubelgiji kwa matibabu alishambuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.

Mara baada ya kushambulia, mwanasiasa huyo  alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma na usiku wa siku hiyo alihamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya alikopata matibabu hadi Januari 6, 2018 na kuhamishiwa  Ubelgiji kuendelea na matibabu zaidi.

Lissu ambaye kwa sasa anatembea kwa msaada wa gongo moja akizungumza na wapiga kura wake mwishoni mwa wiki kupitia simu ya Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amesema anarudi nchini Septemba 7, 2019.

Amesema katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika Oktoba, 2019 atakuwepo Tanzania.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527