MAITI YACHOMOKA KWENYE JENEZA WAKATI WA MAZISHI

Familia chini Ghana huwapa mkono wa buriani wapendwa wao waliofariki dunia kwa mtindo wa aina yake huku wengi wao hata wakiwaajiri kwa muda wasakata densi kushiriki majira ya mwisho ya kumpa buriani marehemu.

 Mtindo huu wa kuwaajiri watakaolibeba sanduku la maiti huku wakisakata densi kwa nyimbo umeonekana kushika kasi mno na ni bayana kuwa utakuwepo kwa muda mrefu zaidi. 

Hata hivyo, kwenye tukio moja mambo yameonekana kwenda mrama katika hafla ya mazishi.

 Katika video moja iliyosambaa kwa kasi mitandaoni, jamaa wa marehemu wameachwa na mshtuko baada ya maiti ya mpendwa wao kuteleza na kuanguka kutoka katika sanduku lililombeba.

 Hii ni baada ya wanadensi waliokuwa wamelibeba sanduku hilo kupoteza mwelekeo wakila uhondo na kupelekea maiti kuchomoka kwa bahati mbaya na kuanguka. 

Familia ya mwendazake na waombolezaji walisika wakimaka kwa mshangao kufuatia kihoja hicho huku jamaa hao wakiwa katika harakati ya kuufunika mwili wa marehemu.
Via>>Tuko

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527