KC,UZALENDO KWANZA KUWAMILIKISHA WASANII ARDHI


Mwenyekiti wa kundi la Uzalendo Kwanza na Mugizaji wa Filamu Nchini, Steve Nyerere akiongea na Waandishi wa Habari juu ya Makubaliano ya Wasaniii wa kampeni ya uzalendo kwanza na kampuni ya KC Land Development Plan Ltd Juu ya Mpango wao wa kukopeshwa Viwanja kwa gharama nafuu pasipokuwa na riba. Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya KC Land Development Plan Ltd,Khalid Mwinyi akitoa maelezo juu ya mradi na Viwanja vitakavyojulikana kama mji wa Wasanii. Msaniii wa na Meneja wa Bendi ya Twanga Pepeta, Luiza Mbutu akieleza ni namna gani bendi yake itakavyotumbuzi siku ya chakula cha pamoja baina ya Wasanii na Kampuni ya KC Land Development Plan Ltd. Msanii mkongwe wa Filamu nchini Chick Mchoma akieleza faida za wasanii watakaochukua Viwanja vya Kampuni ya KC Land Development Plan Ltd ambavyo vinalipwa ndani ya miaka miwili kwa gharama nafuu. Msanii mMahaurufu wa mvchezo wa Bongo Dar es Salaam, Kuwa Kikumba maharufu kama Dude akieleza nini kama wasanii watakwenda kufanya kuhakikisha kuwa wanamiliki viwanja hivyo.  Promota wa Mchezo wa Ngumi ambaye ni Mwanachama wa kundi la Uzalendo kwanza akieleza faida za Viwanja hivyo kwa mabondia ambao wamekuwa wakipata pesa na kufanya anasa pasipo kumiliki ardhi. Msanii wa kike wa Siku nyingi Maya akieleza namana wasanii wakike watakavyokwenda kumiliki nyumba zao na kuacha kunyanyasika. Wasanii kwa pamoja wakiwa wamesimama kama ishara ya kumkumbuka Mzee Reginald Mengi aliyetutoka usiku wa kuamkia leo.Sehemu ya Waandishi wa habari walioshiriki mkutano huo wakitimiza majukumu yao kama wanavyoonekana pichani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post