JESHI LA YEMEN LATEKELEZA MASHAMBULIZI MAPYA YA KULIPIZA KISASI SAUDIA

Jeshi la Yemen limetekelza mashambulizi mapya ya kulipiza kisasi katika eneo la Jizan, kusini magharibi mwa Saudi Arabia.

Televisheni ya Al Masirah imeripoti leo Jumapili kuwa, Jeshi la Anga la Yemen na kamati za wananchi zimetumia ndege isiyo na rubani au drone kushambulia maeneo ya kuegeshea ndege za kivita za Saudia katika uwanja wa ndege wa Jizan.


Taarifa zinasema kuwa oparesheni hiyo imetekelezwa na drone ya kivita ya Yemen aina ya Qasef-K2 baada ya oparesheni ya upelelezi.

Hali kadhalika Jeshi la Yemen limetangaza kuitungua ndege ya kijasusi ya adui katika eneo la mashariki mwa Jabal al-Dudud katika eneo la Jizan.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527