BASI LA KILIMANJARO EXPRESS LAPINDUKA MKOANI TANGA


Basi la abiria la Kampuni ya Kilimanjaro Express limepata ajali eneo la Mkata, mkoani Tanga leo Jumapili Mei 5, 2019.

Mkuu wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Tanga (RTO), Solomon Mwangamilo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kubainisha kuwa basi hilo limepinduka.

“Ni kweli kuna basi la Kilimanjaro Express limeacha njia na kupinduka eneo la Mkata, kwa sasa ndio naelekea eneo la tukio.

“Hatujafahamu hasa ni madhara gani yaliyotokea huko mpaka nikifika huko mwendo wa dakika 45 hivi nitawafahamisha hali halisi,” amesema Mwangamilo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post