ANUSURIKA KUFA BAADA YA KUJIKATA UUME KWA WEMBE

Jamaa kutoka kijiji cha Bula, kaunti ya Isiolo  nchini Kenya aliripotiwa Jumatano kujikata uume wake, akitumia wembe baada ya kuzidiwa na dawa za kulevya. 


Kwa mujibu wa ripoti ya eDaily, mamake jamaa huyo alifichua kwamba kisa hicho kilitokea wakati mwanawe huyo wa miaka 27, Abshiro Abdi, alikuwa akizikata kucha zake. 

 Kwa sasa, abdi anapokea matibabu katika hospitali ya rufaa ya Isiolo. 

Msimamizi wa hospitali hiyo Daktari Hussain Abdi Mohamud adokeza kwamba, mwathiriwa alikuwa amepoteza fahamu alipowasilishwa katika kituo hicho cha afya na kuwa alikuwa ametumia dawa za kulevya kupita kiasi.

 "Alivuja damu nyingi...lakini atakapopata nafuu bado atakuwa na uwezo wa kujisaidia kama kawaida. Nguvu zake za kiume hazitaathirika lakini iwapo kutakuwepo na uwezekano basi madaktari wa upasuaji watamshughulikia kwa njia nyingine ile," Daktari Mahamud alisema. 

Wakati uo huo, alitoa wito kwa vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya akisema kuwa wanahatarisha maisha yao. 

"Vijana wanapaswa kujiepusha na dawa za kulevya za aina yoyote ile, la si hivyo, watazidi kuhatarisha maisha yao, afya yao na mawazo yao pia yataathirika," aliongeza.

Chanzo - Tuko

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527