MAMA AAMUA KUMZALIA MTOTO MWANAWE SHOGA

Mwanamke mmoja nchini Marekani amejifungua mjukuu wake wa kike ambaye alikuwa amembebea kwa miezi tisa mwanawe ambaye ni shoga. 

Kwa maneno rahisi ni kwamba, mtoto wa kiume wa mwanamke huyo ni shoga na mama yake kubeba mimba ilikuwa ndiyo njia ya rahisi kwa 'mume na mke' wake kupata mtoto. 

Matthew Eledge, 32, na Elliot Dougherty, 29, walimkaribisha mtoto wao ulimwenguni kwa jina Uma Louise Dougherty -Eledge baada ya mama ya Mathew, Cecile Eledge kuchukua jukumu la kuibeba mimba hiyo.

 Katika ripoti ya CNN, mama huyo alipata ujauzito kupitia njia ya kitaalamu na Mathew aliwasilisha mbegu ya kiume naye dada ya 'mke' wake Lea Yribe akawasilisha yai. 

"Wakati wewe ni shoga na umeolewa na unataka kuwa na mtoto, ni lazima kufahamu utahitaji njia maalum ya kujenga familia," Matthew alisema kupitia mahojiano na CNN. 

Mama huyo, 61, alijifungua Uma Louise jijini Omaha, Nebraska wiki moja iliyopita na mtoto huyo aliwa na uzani wa kilo 2.6.

 Kulingana na Mathew, mwalimu, walijaribu njia nyingi lakini zilizokuwapo zilikuwa ghali mno na hawakufahamu wafanye nini.

 "Nilikuwa na watu wengi chuoni waliosema (wangezaa mtoto), lakini wakati ukifika, ni jukumu kubwa," Matthewalisema.

 "Zaidi ya yote, tunahisi wenye bahati kubwa kupata wanawake wakarimu sana wanaoweza kufanya hivyo," alisema. 

Wawili hao walisema wana shukrani tele kwa kuwa na familia zenye kujali zaidi na zilizo tayari kuwasaidia kwa lolote.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post