BUNGE LARIDHIA KUTOFANYA KAZI NA CAG KWA KUDHALILISHA BUNGE


Bunge limepitisha azimio la kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.

Uamuzi huo umepitishwa leo Jumanne Aprili 2, 2019 baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, Emmanuel Mwakasaka kuwasilisha na kusoma bungeni taarifa ya kamati hiyo iliyomhoji CAG, kumtia hatiani baada ya kubaini kauli aliyoitoa kuwa Bunge ni dhaifu, amelidhalilisha Bunge.

Naibu Spika, Dk Tulia Ackson alitoa nafasi kwa wabunge kujadili jambo hilo huku wabunge wakipishana maoni yao, kukubaliana na uamuzi huo na wengine kupinga akiwemo Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe.


Baada ya wabunge kutoa maoni yao, Dk Tulia amelihoji Bunge kuhusu hoja hiyo, akiwakata wanaokubaliana na jambo hilo kusema ndio na wasiokubaliana na suala hilo kusema sio, "waliosema ndio wameshinda. "

Na Fidelis Butahe, Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527