RAIS MAGUFULI AIONGEZEA MUDA WA MIAKA 3 BODI YA UTALII TANZANIA (TTB)


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameongeza muda wa miaka 3 kwa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) iliyokuwa imalize muda wake leo tarehe 23 Aprili, 2019.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa Mwenyekiti na Wajumbe wote wa bodi hiyo  wameongezewa muda hadi tarehe 23 Aprili, 2022.

Bodi hiyo inaongozwa na Mwenyekiti, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo na wajumbe 6 kama ifuatavyo;
  1.     Bw. Augustine Kungu Olal.
  2.     Bi. Zabein Muhaji Mhita.
  3.     Bw. Richard Rugimbana.
  4.     Bw. Mark Leveri.
  5.     Bw. Ally Hussein Laay.
  6.     Bw. Ibrahim Mussa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527