POLISI NJOMBE YAUA MAJAMBAZI WAWILI, MMOJA ATOROKA

Na Amiri kilagalila-Njombe

Jeshi la Polisi Mkoani Njombe limefanikiwa kuwaua majambazi wawili kati ya watatu waliokuwa wakijaribu kupora mali kwa kutumia Jambia,kisu na Panga.

Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoa wa Njombe ACP Salum Hamduni,amesema tukio hilo limetokea kijiji cha Lupembe wilayani Njombe  April 28 majira ya saa 01:40 usiku ambapo watu wasiofahamika walivamia nyumba ya Esau Muhavile kwa kuvunja geti na mlango kwa kutumia Spring ya gari na kuingia ndani kwa nia ya kupora mali.

"Awali majira ya saa 01:30 usiku mlinzi aitwae Linus Matimbwi akiwa Lindoni alisikia vishindo vya watu kuzunguka nyumba hiyo na kumgongea Baraka mayemba mfanyakazi wa Esau na kumweleza kuwa huku nje hali si shwari ndipo Baraka akaamua kumpigia simu mkuu wa kituo kidogo cha polisi Lupembe kwa msaada"alisema kamanda.

Amesema kuwa Polisi waliwahi kufika katika eneo la tukio na kugundua kuwa majambazi hao wapo ndani na kupiga Risasi hewani kuwataarifu kuwa wapo chini ya ulinzi lakini hawakutii amri na matokeo yake jambazi mmoja wapo alirusha jambia na kumjeruhi mkuu wa kituo begani kitendo kilichopelekea Polisi kumpiga Risasi kifuani jambazi Newton Mbanga aliyerusha jambia huku Leonard Alphonce akipigwa risasi kichwani na kusababisha vifo vyao.

"Mbinu iliyotumika na majambazi hao ni kuvunja mlango kwa kutumia spring ya gari na kuingia ndani kwa nia ya kupora mali/pesa na watuhumiwa ambao ni majambazi wawili kati yao walifariki dunia na mmoja alifanikiwa kutoroka,na jeshi la polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa huyo" aliongeza kusema kamanda.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527