MIKONONI MWA POLISI KWA KUKUTWA NA NYARAKA ZA SERIKALI

Na Amiri kilagalila-Njombe

Kijana aliyefahamika kwa jina la Ford Abel mwakatundu  (28) mkazi wa makambako mkoani Njombe anashikiliwa na polisi kwa makosa ya kukutwa na nyaraka za serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Salum Hamduni,amesema kijana huyo anashikiliwa kwa makosa hayo kinyume na taratibu za kisheria.

"Mnamo April 22 majira ya saa 12:30 huko Makambako alikamatwa Ford Abel mwakatundu kyusa mwenye umri huo mkazi wa mwembetogwa Makambako kwa kosa la kughushi nyaraka mbali mbali za serikali ikiwemo leseni za kuendesha magari,Tin number, Bima za magari pamoja na nyaraka za sumatra zanazohusiana na Rout za mabasi na magari madogo ya biashara" alisema Hamduni

Ameongeza kuwa nyaraka hizo alikuwa akighushi na kuziuza kwa watu mbali mbali kwa kiasi cha Tsh 100,000/= kwa lengo la kujipatia kipato.

Kamanda amesema upelelezi unaendele na atafikishwa mahakamani pindi upelelezi utakapokamilika.

Meneja wa TRA  mkoa wa Njombe Musib shaaban ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia za kutumia njia za mikato kutafuta kipato kwa kuwa njia hizo zimekuwa zikikwamisha juhudi za serikali.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527