MWANAMKE AELEZA JINSI ALIVYOPATA MIMBA BILA KUFANYA MAPENZI


Mwanamke mmoja wa miaka 23 kutoka Nigeria ameelezea jinsi alivyopata mimba bila kushiriki ngono na mpenzi wake.

 Wathoni Anyansi ambaye alidai kuwa bikira kwa wakati huo, alisema aligundua yuko mjamzito akiwa na miezi mitano.

 Anyansi alishangazwa ni vipi alivyopata mimba hiyo kwani hakuwa ameshiriki ngono ila alibusiana tu na mpenzi wake wakiwa uchi chumbani mwake. 

 "Nilikuwa bikira nikiwa na umri wa miaka 23, niligundua baada ya miezi mitano kwamba nilikuwa mjamzito," Ayansi alisema.

 Ayansi alisema hakuona hedhi kwa miezi mitano, jambo lililomfanya awe na wasiwasi kwani pia alianza kukonda bila ya kuugua ugonjwa wowote.

 Alimfahamisha mamake ila pia alishangazwa ni vipi maajabu hayo yalivyotendeka. 

 Ayansi alisema hakuona hedhi kwa miezi mitano, jambo lililomfanya awe na wasiwasi kwani pia alianza kukonda bila ya kuugua ugonjwa wowote. 

Nilishangaa haya yalitokea kivipi? nilipomwelezea mamangu hakuwa na jambo la kusema ila alicheka tu," Anyansi aliongezea.

 Aidha, wataalam kutoa Uingiereza wanadai kuwa kuna uwezakano mkubwa kwa mwanamke kupata mimba bila ya kushiriki ngono.

 Kwa mara nyingi jambo hili hutokea pale ambapo mwanaume anamwaga mbegu karibu na sehemu za siri za mwanamke.
Chanzo - Tuko

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527