JESHI LILILOMPINDUA RAIS OMAR AL- BASHIR LATOA MAAGIZO KWA BENKI KUU YA SUDAN


Baraza la Kijeshi linaloongoza serikali ya mpito nchini Sudan limeiamuru Benki Kuu ya nchi hiyo, kuchunguza shughuli zote za uhamishaji wa fedha zilizofanyika kuanzia Aprili 1, na kushikilia fedha zote zinazotiliwa shaka. Hayo yameripotiwa leo na shirika la habari la Sudan, SUNA. 

Baraza hilo pia limeamuru kusimamishwa kwa shughuli ya kubadilishwa umiliki wa hisa, hadi itakapotangazwa vinginevyo. 

Benki Kuu vile vile imeamuliwa kuripoti kwa mamlaka husika, juu ya kufanyika mchakato wowote wa uhamishaji mkubwa, au unaotiliwa shaka ya hisa pamoja na umiliki wa makampuni.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post