MTANGAZAJI WA CLOUDS FM EPHRAIM KIBONDE KUZIKWA DAR


Mazishi ya aliyekuwa mtangazaji wa Kituo cha Redio Clouds Fm, Ephrahim Kibonde yatafanyika Jumamosi wiki hii.


Mwili wa Kibonde unatarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam leo Alhamisi Machi 7,2019 saa nne usiku katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere na kuzikwa Jumamosi.

Joseph Kusaga, Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group ametoa taarifa hiyo leo tarehe 7 Machi 2019 na kwamba, mwili wa Kibonde unatarajiwa kutua Dar es Salaam saa 4 usiku wa leo.

Amesema, baada ya kufika mwili huo utahifadhiwa katika Hospitali ya Jeshi Lugalo.

“Jana usiku niliongea na daktari Derrick aliyekuwa anamtibu Ephraim Kibonde akanihakikishia kuwa anaendelea vizuri lakini bahati mbaya wakati tunajiandaa kurudi Dar es Salaam hali ikabadilika na kusabaisha kifo chake.

“Taratibu za mazishi na maombolezo, zitafanyika kesho nyumbani kwake Mbezi na tunatarajia kuaga na kumpumzisha siku ya Jumamosi,” amesema Kusaga.

Soma zaidi hapa : MTANGAZAJI WA CLOUDS FM KIBONDE AFARIKI...ALIKUWA MC KWENYE MSIBA WA RUGE

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527