SUMAYE AUGUA GHAFLA KWENYE ZIARA YA CHADEMA TANGA


 Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ameugua ghafla akiwa mkoani Tanga.

Sumaye ambaye ni mjumbe wa kamati kuu ya Chadema amepatwa na tatizo la afya akiwa katika majukumu ya kichama.

Taarifa iliyotolewa leo mchana Ijumaa Februari 8, 2019 na Mkuu wa Idara ya Mawasiliano na Habari wa Chadema, Tumaini Makene imesema, “Sumaye alikuwa mkoani Tanga, akiendelea na ratiba ya ziara ya shughuli za chama kabla ya kupatwa na shida ya afya ghafla leo asubuhi.”

“Baada ya kutibiwa hali yake inaendelea vizuri na sasa amepumzika wakati mipango ya kumsafirisha kwenda Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo hii kwa ajili ya uchunguzi zaidi ikifanyika.”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527