EBITOKE AKIRI KUBEBA MUME WA MTU


Msanii wa kike wa vichekesho nchini, Annastazia Xavery maarufu kama Ebitoke, hatimaye amefunguka juu ya tuhuma za siku nyingi za kuwa na mahusiano ya kimapenzi na bosi wake, director Timoth.

Akizungumza na Big Chawa kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Ebitoke amefunguka kwamba yeye hakumfuata Timoth ili kuwa naye kwenye mahusiano, licha ya kuwa Bosi wake huyo ni mume wa muigizaji mwenzake, Mama Ashura.

Baada ya kuulizwa tetesi za kugombana na Mama Ashura kwa kumchukulia mume, Ebitoke alikiri haya. “sasa ananimind mimi ndio nilimfuata Timoth nikamwambia njoo kwangu, Haya mambo yalishapitwa na wakati”.

Tetesi za etioke kuwa na mahusiano na Timoth Conrad zilikuwapo kwa muda mrefu lakini wawili hao wamekuwa wakikanusha, na pia kutajwa kuwa ndio chanzo cha Ebitoke kuapa kutorudi Timamu hata apigwe na maisha kwa kiasi gani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527