BABA MZAZI AWAPACHIKA MIMBA MABINTI ZAKE WAWILI

 Baba wa mabinti wawili mjini Eldoret nchini Kenya anasakwa na maafisa wa polisi baada ya kuwabaka na kuwapachika mimba watoto hao kwa wakati tofauti.

Baba huyo anasemekana kuanza kuwabaka wanawe mwaka wa 2014 mama yao alipoaga dunia.

 Mshukiwa alikuwa amerejea nyumbani kutoka gerezani baada ya kukamatwa kwa kumbaka binti wake kitinda mimba.

 Kulingana na taarifa za Citizen TV, jamaa huyo alipofika nyumbani kwake, alimbaka tena bintiye mkubwa ambaye kwa sasa amempachika pia mimba. 

 Msichana huyo aliwambia wanahabari kuwa dadake mdogo alijitoa uhai mwaka wa 2018 akiwa na ujauzito wa miezi saba. 
Msichana huyo ambaye pia ni mjamzito, alisema aliwasilisha malalamishi yake kwa wazee wa kijiji ila hakuna hatua ambayo imechukuliwa dhidi ya baba yao

 Aliamua kuranda katika mitaa ya mji wa Eldoret ila wasamaria wema wajitokeza na kumpa makazi.

Wasichana hao wamekuwa wakiteseka mikononi mwa baba yao ambaye anapaswa kuwalinda tangu mama yao alipofariki mwaka wa 2014.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527