MWALIMU MKUU ATUPWA JELA KWA WIZI WA FEDHA ZA SHULE

Mwalimu Mkuu shule ya sekondari Mikwambe, Paulo Lorry, amehukumiwa kifungo cha miaka sita na kutakiwa kulipa Sh milioni 16 katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke alizoiba kutoka akaunti ya shule.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Taasisiya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) mkoa wa Temeke, Pilly Mwakasege, ilieleza kuwa mwamu Lorry amekutwa na hatia na kuhukukiwa kwenda jela.

Ilieleza kuwa mwalimu huyo alishtakiwa na makosa matatu ya matumizi mabaya ya ofisi kifungu cha 31 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11/2007 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Mshitakiwa alikuwa ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Mikwambe Manispaa ya Temeke mwaka 2010 alipokea Sh milioni 28 kupitia akaunti ya shule namba CA 2011100236 kwa ajili ya ujenzi wa maabara shuleni hapo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527