MDEE AITWA POLISI

Mbunge wa Kawe (Chadema), Halime Mdee ameitikia wito wa Polisi Kinondoni jijini Dar es Salaam aliotakiwa kufika leo Jumamosi Februari 23,2019.

Mdee kupitia akaunti yake ya Twitter ameandika, “Nimepata wito wa kuitwa Polisi Oysterbay kwa mahojiano.”

“Mpaka sasa sababu ya wito ni nini. Ngoja tujongee.”

Baada ya ujumbe huo, Mwananchi limezungumza na Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha) kujua kama amekwisha kufika na kujibu kwa ujumbe mfupi wa maandishi, “Niko kwa RCO. Nimepokelewa, Namsubiri.”
Chanzo - Mwananchi





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527