WANAOMTUKANA RAIS MAGUFULI SASA KUSAKWA HADI WHATSAPP


Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amelitaka jeshi la polisi kwa kushirikiana na TCRA kuhakikisha mtu yoyote atakaye mtukana, kumdhihaki, ama kufanya uchochezi dhidi ya Rais Dkt John Magufuli achukuliwe hatua mara moja.

Akiongea leo ofisini kwake jijini Dar es salaam, Kangi amesema, "wanaomtukana Rais kuanzia sasa wasakwe popote pale walipo wakamatwe".

''Haiwezekani Rais akatukanwa, haiwezekani kabisa, iwe kwenye magroup ya WhatsApp, iwe kwenye ujumbe mfupi wa simu au blog na hata aina yoyote ya mawasiliano wachukuliwe hatua za kisheria'', amesisitiza.

SIKILIZA HAPA CHINI

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527