KIGWANGALLA AFIWA NA MTOTO WAKE..ZITTO KABWE ATOA POLE

Waziri wa Maliasili na Utalii Hamis Kigwangalla amefiwa na mtoto wake anayefahamika kwa jina la Zul, ambapo mazishi yatafanyika kesho saa 10 Wilayani Nzega kwa sasa msiba upo nyumbani kwa Waziri makumbusho nyumba za Mawaziri.

Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe ameonyesha kuguswa na msiba huo na kuandika “Nimepata maumivu makali baada ya kusikia taarifa ya msiba wa mtoto Zul Hamis Kigwangala. Inna Lillah waina ilaih raajiun. Pole sana kwa msiba ndugu yangu Hamis Kigwangalla na mola akupe subra katika mtihani huu mkubwa, mzito sana. Tupo pamoja nawe. Tumshukuru Allah kwa yote”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527