SPIKA NDUGAI : ZITTO KABWE ANANIPA TABU


 Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema mbunge anayempa shida pale anapotaka kumwadhibu ni Zitto Kabwe.

Ndugai ametoa kauli yake hiyo leo Alhamisi Januari 17, 2019 katika mkutano na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam.

Ndugai amesema amekuwa akichelea kumfukuza bungeni mbunge huyo wa Kigoma Mjini kwa kuwa ndiye pekee anayewakilisha Chama cha ACT-Wazalendo.

"Unajua niseme ukweli, huyu mbunge amekuwa akinipa tabu sana, ananipa tabu sababu ndio mbunge mmoja wa chama chake,” amesema Ndugai.

“Hawa wengine huwa nafukuza sababu wenzao wapo, sasa huyu (Zitto) ni mmoja tu wa chama chake (ACT Wazalendo).”

Na Kelvin Matandiko Mwananchi 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527