WALINDA AMANI WAUAWA NA WAPIGANAJI WA AL QAEDA MALI

Wapiganaji wa kiislamu wenye mafungamano na Al Qaeda wamefanya shambulio kaskazini mwa Mali katika kambi ya Umoja wa Mataifa na kusababisha vifo vya Walinda amani 10 raia wa Chad.

Katika shambulio hilo wapiganaji wengine 25 walijeruhiwa,
Wapiganaji hao wamesema shambulio hilo wamelifanya kujibu ziara ya Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu nchini Chad, na pia uamuzi wa Rais Idriss Deby kuanzisha mahusiano ya kidiplomasia na nchi hiyo.

Katika shambulio hilo la Jumapili, wapiganaji hao wenye msimamo mkali walitumia gari la magari ya mizigo na silaha nzito kushambulia kambi ya Umoja wa Mataifa iliyoko kaskazini mwa mji wa Kidal.

Mkuu wa kikosi cha Umoja wa Mataifa nchini Mali Mahamat Saleh Annadif ameliita tukio hilo kama tendo la uhalifu.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527