TETESI ZA SOKA ULAYA , INTER MILAN WAMTAMANI ASHLEY YOUNG

Inter Milan wanamnyatia beki kamili wa Manchester United Ashley Young, 33, na wanatumai kwamba wataweza kumchukua bila kulipa ada yoyote mwisho wa msimu baada ya mkataba wake kumalizika. (Mirror)

Meneja Unai Emery amesema Arsenal bado hawajazungumzia uwezekano wa kumnunua beki wa kati wa Chelsea Gary Cahill, 33, Januari. (Football.London)

Lakini meneja wa Fulham Claudio Ranieri amekuwa wakimtaka Cahill akitumai kumtumia kuimarisha safu yake ya ulinzi Craven Cottage. Anamtaka kwa mkopo wa miezi sita. (The Sun)

Emery amefahamishwa kwamba Arsenal hawataunga mkono mpango wake wa kutaka kuwarejesha Calum Chambers, 23, na Reiss Nelson, 19, mwezi huu. Wawili hao wako nje kwa mkopo. (Metro)Gary Cahill

Chelsea wanakariiba sana kukamilisha usajili wa kiungo wa kati Mmarekani Christian Pulisic, 20, kwa £45m kutoka Borussia Dortmund. (Express)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527