TUME YA UCHAGUZI YAMTANGAZA TSHISEKEDI KUWA MSHINDI WA URAIS CONGO

Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini Congo (Ceni) imetangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo yanayoonesha mgombea wa upinzani Felix Tshisekedi ameshinda kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Desemba 30 mwaka uliopita.


Tshisekedi amemshinda mgombea mwingine wa upinzani Martin Fayulu, pamoja na mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na serikali ya Rais anayemaliza muda wake, Emmanuel Shadary.


Kwa mujibu wa Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Ceni) Corneille Nangaa, mapema leo Alhamisi amesema kwamba kwamba Bw Tshisekedi amepata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa na kumtangaza rasmi kuwa Rais mteule wa nchi hiyo yenye utajiri mkubwa wa madini na mafuta.


Tshisekedi anatokea katika muungano wa kisiasa na aliyekuwa mgombea wa chama cha UNC (Union for the Congolese Nation), Vital Kamerhe ambaye atakuwa ni Waziri Mkuu wa serikali yao kwa mujibu wa makubaliano yao.


Ripoti zinaeleza kuwa mshindi wa kwanza (Felix Tshisekedi) amepata kura takriban milioni 7, huku mshindi wa pili (Martin Fayulu akipata kura takriban milioni 6.4 milioni na mgombea wa tatu ambaye anaungwa mkono na Rais Joseph Kabila (Emmanuel Ramazani Shadary) akipata takriban kura millioni 4.4.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527