AZAM FC YATINGA NUSU FAINALI MAPINDUZI..YAITWANGA MALINDI 2 - 1


Azam Fc imefanikiwa kutinga nusu fainali katika michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kuichapa Malindi FC mabao 2-1.

Mechi hiyo imepigwa usiku huu kwenye Uwanja wa Amaan Zanzibar.

Kutokana na ushindi huo Azam FC inatinga nusu fainali na kuikwepa Simba SC.

Mabao ya Azam Fc yamefungwa na Agrey Morris pamoja na
Donald Ngoma huku bao la Malindi FC likifungwa Abdulswamad Kassim

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527