TETESI ZA SOKA ULAYA JAN 10 2018

Kiungo wa kati wa Arsenal na Wales Aaron Ramsey, 28, amekubali kujiunga Juventus mwezi Juni mwaka huu. (Guardian)


Atletico Madrid imeingia katika kinyang'anyiro cha kumsajili kwa mkopo mshambuliaji wa Chelsea na timu ya taifa ya Uhispania Alvaro Morata, 26.

Kuna tetesi kuwa Morata huenda akajiunga na Sevilla. (Goal)

Real Madrid wanajiandaa kutoa ofa ya euro milioni 9 kumenyana na mahasimu wao Manchester United katika juhudi za kumnunua mlinzi wa Napoli na Senegal Kalidou Koulibaly, 27. (Il Mattino, via Talksport)

Azma ya United ya kumnunua mlinzi wa Fiorentina na Serbia Nikola Milenkovic, 21, huenda imefifia baada ya Jose Mourinho kutimuliwa kutoka klabu hiyo. (ESPN)

Burnley wanakadiria kuwa thamani ya mlinzi wa England James Tarkowski, 26 ni euro milioni 50 japo Liverpool wanapania kumchukua kiungo huyo kwa mkopo. (Sun)

Mchambuliaji wa Southampton, mtaliano Manolo Gabbiadini, 27, amekubali kujiunga tena na Sampdoria kwa kima cha euro milioni 11.7. (Guardian)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527