WENGER KUREJEA KWENYE UKOCHA MICHUANO YA KOMBE LA DUNIA 2022

Arsene Wenger.

Meneja wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger anajipanga kurudi katika kazi yake ya ukocha, huku ripoti zikieleza kuwa ataifundisha Timu ya Taifa ya Qatar katika kuelekea michuano ya Kombe la Dunia la 2022.

Wenger amehusishwa na tetesi kadhaa za kufundisha timu mbalimbali zikiwemo PSG, Real Madrid tangu alipoondoka Arsenal mwishoni mwa msimu uliopita, akisisitiza kuwa anahitaji changamoto mpya na kwamba Qatar inajipanga kuchukua fursa ya hali hiyo na kumvuta mfaransa huyo.

Kwa mujibu wa mtandao wa France Football, Qatar inajipanga kumnyakuwa kocha huyo kwaajili ya maandalizi ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2022 ambayo itafanyika nchini humo.

Habari za maslahi ya Qatar hutoka kwa Soka la Ufaransa, ambao wanasema kuwa Qatar ni nia ya kurekebisha timu yao ya kitaifa ya kuweka mbele ya Kombe la Dunia ya 2022.

Kocha huyo alinukuliwa miezi kadhaa iliyopita, akisema kuwa anatamani kurejea katika kazi yake mapema mwaka huu 2019 baada ya kuwa amepumzika kwa kipindi cha kutosha.

Arsene Wenger (69) alihudumu miaka 22 na klabu ya Arsenal, akiiongoza klabu hiyo kushinda mataji matatu ya EPL na mataji saba ya FA.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527