RAIS TRUMP AKAZIA UJENZI WA UKUTA, ALITAKA BUNGE KUIDHINISHA DOLA BILIONI 5.7

                     Rais wa Marekani Donald Trump.

 Rais wa Marekani Donald Trump wanawake na watoto ni waathirika wakubwa wa mfumo ulioharibika kukabiliana na usafirishaji haramu wa watu akisema idara za doria mpakani hazina tena nyumba za kuwapatia hifadhi wahamiaji na haziwezi kuendelea na utaratibu kwa watu wanaotafuta hifadhi.

Trump anasema kuna mzozo wa kibinadamu na usalama unaoendelea kuwa mkubwa kwenye mpaka wa Marekani na Mexico akiueleza kuwa ni mzozo wa moyo na kiroho.

Katika hotuba yake ya kwanza ya kitaifa kutoka chumba cha Oval Office ndani ya White House Rais Trump alifafanua hoja yake ya kujenga ukuta kwenye mpaka wa Marekani na Mexico lakini hakutangaza hali ya dharura ya kitaifa ambayo itamruhusu kujenga ukuta bila idhini ya bunge.


Alisema wakati wamarekani wanaumizwa kutokana na kile alichokieleza kutodhibitiwa wahamiaji haramu Rais Trump alisema wamarekani wenye asili ya Kiafrika na asili ya Amerika Kusini wanaathirika zaidi kwa sababu fursa za ajira zimechukuliwa na wahamiaji.


Trump alisema wanawake na watoto ni waathirika wakubwa wa mfumo ulioharibika kukabiliana na usafirishaji haramu wa watu akisema idara za doria mpakani hazina tena nyumba za kuwapatia hifadhi wahamiaji na haziwezi kuendelea na utaratibu wote kwa watu wanaotafuta hifadhi.

Chanzo:Voa


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527