RAIS BONGO AREJEA NCHINI BAADA YA JARIBIO LA MAPINDUZI

Rais wa Gabon Ali Bongo anarejea nchini mwake leo Jumanne baada ya kuwa nje ya nchi kwa zaidi ya miezi miwili akipokea matibabu nchini Morocco.


Bw Bongo anarejea wiki moja tu baada ya jeshi nchini humo kufanikiwa kuzima jaribio la mapinduzi ya serikali yake.

Kiongozi huyo mwenye miaka 59 amekuwa akipokea matibabu nchini Morocco tangu Oktoba 24 alipopata kiharisi akihudhuria mkutano mkuu wa kiuchumi nchini Saudi Arabia.

Baada ya utata kuhusu hali yake, makamu wake hatimaye alitangaza mwezi Desemba kwamba alipatwa na kiharusi.

Mara pekee kwake kuonekana na umma ilikuwa ni wakati wa hotuba ya kila mwaka ya Mkesha wa Mwaka Mpya ambayo ilirekodiwa akiwa Morocco.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527