BODI YA MIKOPO HESLB YATANGAZA NJIA MPYA KWA WANAODAIWA MIKOPO


Mkurugenzi wa bodi ya mikopo nchini, Abdulrazack Badru .

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, HESLB imekuja na mfumo mpya wa kielektoniki wa ulipaji madeni ya waliyokuwa wanufaika wa mikopo, ambapo mfumo huo utajulikana kwa jina la 'Goverment Electronic Payment Getway' (GEGP).

Akitangaza mfumo huo, Mkurugenzi wa bodi ya mikopo nchini, Abdulrazack Badru amesema mfumo utarahisisha uwazi wa kwenye ukusanyaji wa fedha hizo, utamfanya mdaiwa kulipa mahali popote alipo pamoja na kutoa fursa ya kuongezeka kwa mapato ya bodi hiyo.

"Tumekamilisha utaratibu mfumo wa serikali wa kukusanya mapato (GEPG), mwajiri na wanufaika watatakiwa kujiunga kwenye mfumo huu mpya wa GEPG ili kulipa madeni wanayodaiwa na serikali," amesema Badru.

Aidha amesema, "waajiri ambao watashindwa kulipa madeni ya wafanyakazi ambao walikuwa ni wanufaika, tutawaanzishia operesheni maalumu ya kupitia maofisini kwao ili kuwabaini wasiolipa mikopo ya bodi".

Akifafanua mfumo huo mpya mtaalamu wa GEPG, Baziri Bajunia amesema, "mfumo huu umekuwa ukitumika sasa hivi na taasisi nyingi ambazo zinafanya malipo kwa taasisi za serikali, ni utaratibu ambao hata taasisi nyingine za kifedha wanautumia".

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527