MBIVU NA MBICHI KUJULIKANA LEO.. UINGEREZA KUJITOA UMOJA WA ULAYA AMA LA

Wabunge Uingereza wanajitayarisha kupiga kura kwa iwapo kuunga au kutounga mkono mpango wa Theresa May wa kujitoa katika Umoja wa Ulaya.


Kura hiyo inayotajwa kuwa  Kura yenye umuhimu itafanyika baadaye leo wakati mjadala wa siku tano kuhusu Brexit ukikamilika.

Bi May amewataka wanasiasa kuunga mkono mpango wake au kuhatarisha kuwavunja moyo raia wa Uingereza.

Lakini huku wabunge wake mwenyewe wakitarajiwa kujiunga na wa vyama vya upinzani kupiga kura dhidi ya mpango huo, inatarajiwa pakubwa kwamba mpango huo hautofaulu.

Wabunge pia watapata fursa ya kutoa mapendekezo ya marekebisho ambayo yanaweza kuunda upya mpango huo kabla ya kura kuanza 19:00 kwa saa ya GMT.

Chanzo:Bbc

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post