MBOWE ANYANG'ANYWA OFISI NA KUPEWA UHAMIAJI

Mwenyekiti wa (CHADEMA) taifa, Freeman Mbowe.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) taifa, Freeman Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, amenyang'anywa Ofisi yake ya Ubunge na Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya na kuagiza itumiwe na Idara ya Uhamiaji.

Ole Sabaya amefikia uamuzi huo kwa kile alichodai kuwa ameelezwa kuwa Mbowe hajaitumia ofisi hiyo tangu mwaka 2010, hivyo haina haja kuendelea kuwepo na kutotumika katika matumizi yaliyo kusudiwa.

"Tangu Mbowe achaguliwe Mwaka 2010 hajawahi kuingia katika Ofisi hiyo kusikiliza kero za wananchi, sijui yupo wapi namsikia huko maeneo mengine akifanya vurugu, sasa ofisi hii itatumika kusaidia wananchi", amesema Ole Sabaya.

Mbowe amenyang'anywa ofisi hiyo akiwa gerezani baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwafutia dhamana Novemba 23, 2018 kwa kukiuka masharti ya dhamana ikiwemo kutoka nje ya nchi bila kibali, yeye pamoja na Mbunge wa Tarime Mjini Ester Matiko.

Mbowe na Matiko wako mahabusu baada ya kufutiwa dhamana kwenye kesi yao ya msingi inayowakabili juu ya kusababisha kifo cha aliyekuwa mwanafunzi wa NIT, Akwilina Akwilini baada ya kufanya maandamano kuelekea katika ofisi za Mkurugenzi wa Kinondoni Februari 2018.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527