MANJI KUSUBIRIWA LEO OFISINI JANGWANI

Makao Makuu ya klabu ya Yanga.

Taarifa hiyo ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini la klabu hiyo ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika, Novemba mwaka uliopita kufuatia sintofahamu juu ya uchaguzi mkuu wa klabu hiyo.

Mkuchika alisema kuwa, Manji aliliambia baraza hilo la wadhamini wa Yanga kuwa tarehe ya leo ndipo ataanza kwenda ofisini kwake Yanga, alipokuwa akijibu barua ambayo aliandikiwa na Baraza hilo.

Ikumbukwe kuwa mchakato wa uchaguzi wa klabu hiyo umesimamishwa na Mahakama kufuatia baadhi ya wanachama kushtaki juu ya mwenendo mzima wa uchaguzi huo ambao ulitakiwa kufanyika wikiendi iliyopita.

Mashabiki na wanachama wa Yanga, wanasubiri endapo Mwenyekiti wao wa zamani, Yusuph Manji atarejea katika nafasi yake hii leo ama la!.

Chanzo:Eatv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527