YANGA YAMALIZA KOMBE LA MAPINDUZI KWA KUICHAPA JAMHURI 3 - 1

Yanga imemaliza mechi yao ya mwisho ya hatua ya makundi katika michuano ya Kombe la Mapinduzi kwa kuichapa Jamhuri kwa mabao 3-1.

Mechi hiyo imepigwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar, leo na timu zilicheza bila ya presha kubwa.

Yanga iliyoonyesha soka safi ilifanikiwa kushinda kwa mabao hayo ualiyofungwa na Faraji Kilaza, Gustafa Saimon.

Hadi mapumziko, tayari Yanga ilikuwa imepata mabao hayo matatu na Jamhuri moja, na kipindi cha pili kikawa hakina mabao.

Kipindi cha pili kilionekana kuwa cha tahadhari kwa kila timu. Licha ya Jamhuri kutaka kusawazisha mabao hayo mawili lakini ilionekana kujilinda kwa kiasi kikubwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527