MAMA AJIFUNGUA WATOTO WANNE KWA MPIGO MWANZA

Picha hazihusiani na habari hapa chini

Jenipher Juma (23), mkazi wa Ibanda jijini Mwanza amejifungua watoto wanne miezi miwili kabla ya siku ya makadirio aliyotarajiwa kujifungua.

Jenipher ambaye huo ni uzao wake wa pili alijifungua mchana wa juzi Jumatano Januari 9, 2019 katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Mwanza ya Sekou-Toure.

Mama huyo amejifungua watoto wawili wa kiume na wawili wa kike ambao hali zao zinaendelea vizuri.

Huo ni uzao wake wa pili baada ya ule wa kwanza wa Aprili, 2018 ambapo pia alijifungua watoto wanne kwa wakati mmoja kwa njia ya upasuaji.

“Bahati mbaya watoto wangu wa kwanza walifia tumboni miezi mitatu kabla ya muda wa kujifungua ikabidi nifanyiwe operesheni,” alisema Jenipher.

Muuguzi kiongozi wa wodi ya wazazi, Tatu Lusesaamesema safari hii Jenipher amejifungua salama kwa njia ya kawaida na watoto wote wanaendelea kuwa chini ya uangalizi maalumu kutokana na kuzaliwa wakiwa chini ya uzito wa kawaida.

Via Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527