TUNDU LISSU AU ZITTO KABWE LAZIMA ASHINDE URAIS 2020 - ADO



Katibu wa Itikadi na Uenezi ACT Wazalendo, Ado Shaibu ameweka wazi kuwa akipewa nafasi ya kuchagua kati ya Tundu Antiphas Lissu (CHADEMA)na Zitto Kabwe (ACT Wazalendo) kugombea urais itakuwa ngoma droo kwa kuwa ni viongozi wenye misimamo na kusimamia kilicho sahihi.

Ado amesema kwamba anaamini kupiti muungano wa vyama vya upinzani uliofanyika, kiongozi yoyote atakayesimamishwa kugombea urais 2020 lazima ashinde.

Akiwachambua viongozi hao wawili kwenye www.eatv.tv, Ado amesema kwamba kutokana na ukaribu wake wa kufanya kazi na Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini na hata kwenye masuala mbalimbali tofauti na kazi anamtambua ni kiongozi mwenye maono makubwa sana na Tanzania hivyo akipatiwa nafasi atafanya mambo makubwa.

Akimzungumzia Lissu ambaye ni Mbunge wa Singida Mashariki, Ado amemuelezea kama Mwanaharakati wa siku nyingi asiyeogopeshwa lakini mwenye uwezo wa kusimama na kuikosoa Serikali ya Rais Magufuli.

"Kwa kufanya kazi nyingi na Zitto Kabwe, naweza kusema Zitto yupo tayari kubeba majukumu makubwa ya kuiongoza Tanzania. Mimi ni zao la Zitto kwenye siasa lakini pia namjua vizuri. Lakini kwa upande wa Lissu namna ninavyomtambua sina budi kusema wote wawili ni ngoma droo", ameongeza Ado.

Mbali na hayo, Ado ameshauri vyama vya upinzani kuwa havipaswi kusimamisha mgombea kila chama bali wanapaswa kuteua kiongozi mmoja atakayepewa nguvu na vyama vingine ili kuweza kuitoa serikali ya CCM madarakani.
Chanzo- EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527