RAIS MAGUFULI AUKUBALI MOTO WA KATIBU MKUU WA CCM

Rais John Magufuli ameweka wazi kuwa hotuba za Katibu mkuu wa CCM Dkt. Bashiru Ally huwa zinamshangaza kwa namna ambavyo anazitoa bila uoga jambo ambalo humfanya yeye ajione ni mpole.



Mwenyekiti huyo wa CCM alieleza hilo jana kwenye hotuba yake wakati wa mapokezi ya ndege ya pili aina ya Airbus A220-300 iliyowasili nchini jana mchana Januari 11, 2019 kwenye Uwanja wa Ndege wa kimataifa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.

''Dkt. Bashiru amekuwa muwazi, huwa namuangalia kwenye hotuba zake saa nyingine nasema kumbe mimi nafuu bwana kuliko huyu jamaa'', alisema.

Rais alieleza kuwa Katibu wake huyo amekuwa akikemea ufisadi ambao ulikuwa ukishamili siku hadi siku lakini sasa yeye anapingana nao hadharani bila kujali.

Magufuli amewataka viongozi wote wa chama na Serikali kuendelea kuwatumikia wananchi kwa moyo mmoja ili kusaidia maendeleo na siku moja Tanzania itakuwa kama Ulaya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527